Ligi Kuu Tanzania Bara VPL: Kubashiri Mtandaoni, Utabiri na Vidokezo kwa Watanzania

Ligi kuu Tanzania Bara ni ligi yenye kiwango cha juu katika mpira wa miguu Afrika Mashariki. Ligi hiyo iliundwa mnamo mwaka 1965 wakati huo ikiitwa Ligi ya Kitaifa kisha baadaye ilibadilishwa na kuitwa Ligi Kuu mwaka 1997.

Soka la Tanzania Upo chini ya Uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF). Ligi yetu ni ligi bora kabisa kwa ukanda wa Afrika Mashariki inayojumuisha jumla ya timu 18, kila timu inakutana mara mbili na timu pinzani nyumbani na ugenini kufanya jumla ya mechi zilizochezwa kuwa 36 hadi mwisho wa ligi.

Timu Bingwa hufuzu kucheza katika Ligi ya mabingwa Afrika wa CAF wakati mshindi wa kombe la Azam Sports Confederation Cup (ASFC) huenda kushiriki kombe la Shirikisho Afrika.

Watanzania wengi wamekuwa na Hamasa sana kwa vilabu vinavyoshiiriki ligi hii kutokana na Uwekezaji ambao umefanywa na baadhi ya vilabu kwa Kufanya Usajili wa gharama kuleta wachezaji mahiri wa ndani na nje ya Afrika.

Vidokezo bora zaidi vya kubashiri ligi kuu ya Tanzania Bara.

Uwe na ujuzi au ufahamu mkubwa, wa kiasi, mdogo au hauna ufahamu wowote kuhusiana na ligi ya Tanzania, Kubashiri katika ligi hiyo pendwa Afrika Mashariki, ondoa shaka! Upo katika mikono salama.

Kabla ya kufanya ubashiri wowote timu ya wataalamu wa kubashiri watafanya utafiti wa kina wa takwimu, historia, hali ya hewa, fomu ya timu, taarifa za kocha, ratiba za mechi, vidokezo vya ubashiri na taarifa zingine mbali mbali muhimu kuhusiana na kubashiri katika ligi ya Tanzania kwa kila wiki ya mechi na kukupatia taarifa hizi BURE kabla hujabashiri.

Ligi Kuu ya Tanzania Bara VPL ina ladha yake kwa mashabiki hasa yale manjonjo waletayo wasemaji wa vilabu huleta hamasa kwa mashabiki kusafiri kuzifuata timu zao. Yote haya utayapata ukiwa na Gal Sport Betting Tanzania kwa kukupa nafasi ya wewe kuweza kubashiri mechi za nyumbani maana watanzania ni washabiki wa kweli.

Timu gani zinashiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Ni timu Kumi na nane kwa sasa zinazoshiriki ligi kuu Tanzania Bara ambazo ni:

1.Azam FC
2.Biashara United
3.Coastal Union
4.Dodoma Jiji
5.Gwambina
6.Ihefu
7.JKT Tanzania
8.Kagera Sugar
9.Kinondoni Municipal Council (KMC)
10.Mtibwa Sugar
11.Mbeya City
12.Mwadui
13.Namungo
14.Polisi Tanzania
15.Ruvu Shooting.
16. Simba SC
17.Tanzania Prisons
18.Young Africans SC

Odds bora zaidi za Ligi kuu Tanzania Bara

Katika kubashiri,chochote kile utakachochagua kubashiri ni muhimu kujikusanyia odds bora #1 nchini, kubashiri Ligi Kuu Bara kwa Gal Sport Betting lipo katika kuhakikisha hili, tembelea tovuti yetu mara kwa mara ushuhudie!

Nani ameshinda mataji mengi zaidi ya Ligi Kuu Tanzania Bara?

Kwa kipindi cha miaka 56 ya Ligi kuu, Miamba ya ‘Jangwani’  maarufu kama Wananchi ndio wanaoshikilia usukani kwa kunyakua mataji mengi zaidi wakiwa na jumla ya mataji 22, huku miamba ya Msimbazi Simba SC wakiwana jumla ya mataji 21, Majimaji wakishikilia nafasi ya tatu kwa mataji 3

Washindi wa hivi Karibuni,

  • 2010–11: Young Africans S.C. (Dar es Salaam)
  • 2011–12: Simba S.C. (Dar es Salaam)
  • 2012–13: Young Africans S.C. (Dar es Salaam)
  • 2013–14: Azam F.C. (Dar es Salaam)
  • 2014–15: Young Africans S.C. (Dar es Salaam)
  • 2015–16: Young Africans S.C. (Dar es Salaam)
  • 2016–17: Young Africans S.C. (Dar es Salaam)
  • 2017–18: Simba S.C. (Dar es Salaam)
  • 2018–19: Simba S.C. (Dar es Salaam)
  • 2019–20: Simba S.C. (Dar es Salaam)

Odds bora zaidi za ligi kuu ya Tanzania Bara

Tunafahamu ni jinsi gani ligi ya Kuu Tanzania Bara inavyosisimua, hivyo jukumu letu haliishii tu katika kukupa dondoo, vidokezo, ushauri na matukio muhimu ya VPL bali tunajiongeza kufanya burudani yako iwe na manufaa maradufu kwa kukupa odds zilizo bora zaidi katika kubashiri Ligi hii Pendwa Afrika Mashariki.

Vidokezo vya kubashiri wakati mechi ya Ligi Kuu Bara inaendelea – Live betting!

Kubashiri moja kwa moja kunakuwa kwa kasi sana na kwa usaidizi wa wataalamu na watafiti wetu ikijumuishwa na jinsi ligi kuu Tanzania bara ilivyokuwa ya kusisimua ndani ya dakika 90 za kila mchezo unakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kujishindia donge nono wakati mechi ikiendelea.

Odds huweza badilika kila mechi inavoendelea kuchezwa na kinachovutia na tunachojivunia zaidi ni uwezekano wa kuweza kupata pesa zako za ushindi ndani ya muda mfupi.

Matokeo ya mechi nzima (Dakika 90)

Kubashiri matokeo ya mechi nzima bado ni njia maarufu zaidi ambayo wabashiri wengi huipenda, yani timu moja kushinda au pengine hata kusuluhu.

Hii ni tofauti na kubashiri idadi sahihi ya magoli ya mechi nzima kama vile 2-1, 3-3, 2-0 na kadhalika.

Odds hubadilika kila wiki kulingana na kila mechi kutokana na fomu au ubora wa timu, ukifuatilia kwa makini uchambuzi wa watalaamu wetu hakuna matokeo ya ligi ya Ligi Kuu Tanzania Bara yatakayo kushangaza.

Timu kufunga magoli na kushinda

Kama ilivyokuwa maarufu kwa njia ya kubashiri mshindi wa dakika 90 wa mchezo, njia ya kubashiri timu zote kufunga magoli nayo imekuwa maarufu zaidi kila kukicha

Ni vizuri kuangalia takwimu na kujua timu yenye kawaida ya kufunga magoli zaidi pia na timu yenye uwezekano mkubwa wa kuruhusu goli au magoli.

Kwa mfano kwenye msimu wa 2019/20 Simba SC ndio timu iliyokuwa na magoli mengi zaidi ikiwa imefunga magoli 78, huku Singida United ikiwa ndio timu iliyoruhusu magoli mengi zaidi ikiruhusu kufungwa magoli 73.

Takwimu hizi na dondoo nyingine nyingi za kukuwezesha wewe kuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kujiongezea faida maradufu ya kiasi cha ubashiri wako utazipata kila unapotembelea tovuti yetu mara kwa mara.

Kufunga goli kwa kichwa

Upana wa kubashiri kuhusu mfungaji wa goli hauishii tu kwenye kubashiri mchezaji gani atafunga goli au atakayeanza kufunga goli bali pia unaweza kubashiri njia ambayo atatumia kufunga goli kama vile goli la kichwa!

Japo ligi kuu Bara si maarufu sana kwa magoli ya kichwa kama ilivyo ligi ya South Africa bado kuna wachezaji machachari ambao hutikisa nyavu kwa style hii ya ufungaji kama vile Meddie Kagere , John Bocco wote kutoka Simba SC

Tembelea tovuti yetu ya Gal Sport Betting Tanzania mara kwa mara kwa ofa kabambe na njia nyingine zaidi ya zilizotajwa hapo juu, ushauri, matukio muhimu, taarifa na vidokezo vya kubashiri kwa uhakika zaidi katika ligi kuu Tanzania Bara